

Huduma ya NENO Kwenye Internet
http://nenosasa.netfirms.com
Tel.
254722410381 E-mail:
jamainga@yahoo.com
Huduma
ya Neno sasa yatinga Nairobi
Mchungaji James Maina Ng'ang'a sasa ametua Nairobi. Kile alichokitamani
siku nyingi sasa kimetimia. Mwenyewe anadai ni wakati wa Mungu umefika
awe na huduma kubwa Nairobi, na hakuna mtu wala shetani atakayezuia
hilo. Akizungumza kuhusu ajali mbaya aliyoipata karibuni, alisema
amejua kwamba zilikuwa mbinu za shetani kumzuia asiingie Nairobi kwa
kishindo. Kanisa lake liko barabara ya uhuru karibu kabisa na mahali
lilipo kanisa la Redeemed ambalo linasimamiwa na Mchungaji Wilfred
Lai. Sijui ilikuwaje, lakini hata Mombasa makanisa ya hawa wachungaji
wawili huwa yamekaribiana kiasi cha kuwafanya watu waamini kwamba
wanashindana. Lakini Ng'ang'a alisema kwamba yeye hashindani na Mtu
bali anayeshindana naye ni Shetani. Kwamba imetokea kupata kiwanja
jirani na kanisa jingine hiyo haina maana kwamba kuna ushindani wowote.
Aliwahurumia wanaodhani kwamba yeye anashindana nao. Alisisitiza kwamba
ni mawazo hayo potovu ndiyo yanayowafanya wengine wampige vita ambayo
yeye hajajiandaa kupambana. Alimaliza kwa kusema wanajisumbua, na
hawatafaulu kwani Mungu ameamua kumwandalia meza machoni pa watesi
wake.
Serikali
Kenya Darubini kwa Ng'ang'a


Kushoto ni Pastor
James Maina Ng'ang'a, wakiwa na kiongozi wa kundi la MUNGIKI.
Mchungaji
Maina Nganga alianzia Mombasa na sasa yuko Nairobi. Kanisa la Mombasa
limefifia huku washirika wakihamia makanisa mengine. Aliyefaidi sana
Mombasa ni mchungaji Panga ambaye washirika wengi wa Nganga wamehamia
kwake. MTAKA YOTE HUKOSA YOTE ndivyo wanavyosema Mombasa. Wengine
wanasema TAMAA ILIMPONZA FISI. Naye mchungaji Nganga anasema sasa
Mungu amemwita Nairobi, na Mombasa ikae. Nayo serikali ya Kenya imekuwa
ikimfuatilia kwa karibu mchungaji Ng'ang'a baada ya kiongozi wa kundi
la Mungiki kudai ameokoka na kujiunga na kanisa la Ng'ang'a. Wanaiona
hiyo kama mbinu ya MUNGIKI kuja na sura mpya ya kanisa la Neno Evangelism.
Wengine wanamlaumu mchungaji Ng'ang'a kwa kujitakia makuu. Wengi wa
washirika wake wanalalamika kwamba matumizi katika kanisa hilo ni
ya juu kiasi kwamba hawawezi kuyamudu. Walitoa mfano wa vipindi katika
redio na TV. Bei zake ni juu sana kwani kila wiki wanalazimika kulipa
KSHS. 70,000 hiyo ni kwa ajili ya vipindi katika vyombo vya habari
tu. Pia walisema kila mwezi hulazimika kulipia nyumba ya Mchungaji
huko Nyali Mombasa na nyingine Runda Nairobi. Nyumba ya Mombasa ni
KSHS 30,000 kila mwezi wakati ile ya Nairobi ni KSHS 40,000 kila mwezi.
Walikumbusha kwamba nyumba hizo lazima zilipiwe miezi mitatu mbele.
Tena walilalamika kuhusu michango ya kununua gari la mchungaji. Kwa
imani mchungaji hupenda kuendesha gari kubwa ya kifahari na ya kisasa
kabisa. Kwa sababu kampuni za magari hutoa magari kila kukicha,
hakuna siku watamaliza kununua gari la mchungaji. Likitoka jipya mchungaji
anasema ataliendesha kwa imani. Imani ya mchungaji inawalazimu washirika
waingie mifukoni kuitimiza imani hiyo. Wengi waliokuwa wakuu katika
mashirika imewabidi wafutwe kazi baada ya mashirika hayo kupata hasara
ya mamilioni ya pesa. Kuna wale wanaosema hasara kwenye mashirika
hayo ilisababishwa na ufujaji wa pesa zilizopelekwa kanisani kulipia
gharama za juu kanisani ambazo hakuna dalili kwamba zitamalizika karibuni.
Ni kweli kila mtu amepewa huduma tofauti na mwingine, lakini tofauti
hiyo ikiwa ni kuwalemea washirika na mahitaji ya pesa yasiyoisha,
tuna mashaka kama na hiyo ni huduma ya Mungu.





Siyo
kweli kwamba wahubiri ni watu waliokosa la kufanya.
Mchungaji James Maina Nganga alikuwa na mengi ya kufanya kabla hajaanza
kuhubiri. Alipotoka jela alianza kuuza kaseti za nyimbo za injili
akitumia baiskeli.

Mchungaji James Maina Nganga, tayari kikazi.

Pasror Mr. and Mrs. James Maina Nganga
"Haki za wanawake ni kubaki wanawake, wakati haki za wanaume
ni kudumu wanaume. Wanawake hawawezi ya wanaume, pia wanaume hawawezi
ya wanawake. Mashindano ya nini kati ya wanawake na wanaume? Kwa nini
wanawake wanatamani kuwa wanaume?"

Pastor James Maina N'gan'ga.
"UPAKO huleta mali, lakini mali haiwezi kuleta UPAKO." Utafuteni
kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.


Mchungaji Maina akiwa na gari yake ya kifahari kabla haijapata ajali.

Huwezi kuamini baada ya ajali hii mbaya Mchungaji Ng'ang'a alitoka
bila majeraha yeyote. huo ni muujiza wa Mungu kwa mtumishi wake. Mwenyewe
amekuwa akihubiri kwamba hatawahi pata ajali maishani mwake. Pengine
ajali hii ni fundisho kwake na kwetu pia. Mungu asifiwe. Kwa sasa
Kanisa la NENO Nairobi linakita mizizi jambo linalozua upinzani mkubwa
kutoka hata kwa wachungaji marafiki zake. Kitonga aliyekuwa rafiki
wa karibu, sasa i8nasemekana ndiye anayepinga kwa nguvu zote kanisa
la NENO kujengwa karibu na NGOME yake Nairobi.







Tangaza
Biashara yako Bure
Tuma picha na maelezo kwa munishifaustin@yahoo.com

http://munishi.com
Send a photo and information
to munishifaustin@yahoo.com